
OPEN CALL OPPORTUNITY
October 17 @ 8:00 am - 6:00 pm

MWITO WA MAOMBI: Mradi wa VIJANA@rtWORK
Je, wewe ni Shirika linaloongozwa na Vijana na uko tayari kutumia utamaduni kama nyenzo ya mabadiliko ya kijamii? Hii ndiyo nafasi yako!
Vigezo vya Ushiriki
– Shirika linaloongozwa na Vijana (YLO)
– Lipo katika moja ya kanda 7 za Tanzania: Ziwa, Magharibi, Kaskazini, Mashariki, Kati, Nyanda za Juu Kusini, Nyanda za Juu Kusini Magharibi
– Kutumia nyenzo za kitamaduni (Sanaa za Jukwaani, Filamu, Redio)
– Kuhusu mada zifuatazo: Usawa wa Kijinsia | Mabadiliko ya Tabianchi | Uhuru wa Kisanii
Ufadhili
Kiasi: EUR 20,000 – 50,000 | Muda wa utekelezaji wa mradi: miezi 12–18
Mahitaji ya Maombi
– Cheti cha Kodi cha 2025
– Taarifa za Fedha Zilizokaguliwa (miaka 2 iliyopita)
– Taarifa ya Benki ya Mwaka wa Sasa
– Katiba na Cheti cha Usajili
– Pendekezo la Mradi + Bajeti ya Kina (PDF)
– Barua 2 za Marejeo (kutoka kwa AZAKi zinazoshirikiana na serikali za mitaa)
Wasilisha maombi yako kupitia www.cdea.or.tz
📅 Mwisho wa kutuma maombi: 17 Oktoba 2025 | Saa 12:00 jioni (EAT)
📩 Kwa maelezo zaidi: info@cdea.or.tz | 0788 348 771
Tujenge mshikamano wa kijamii Tanzania kupitia ubunifu na utamaduni!
#VIJANA@artWORK #cdeatz #goetheinstitut #europeanunion #youthvoices #cultureforchange #socialcohesion #vijanaartwork